ads 728x90 B

Lulu: Sanaa kimeo, sanaa jela, sanaa mafanikio!






Mwandishi Wetu
KIWI cha yule ni chema cha hata ulimwengu uishe. Hiyo ni methali ya Kiswahili ambayo inajibiwa kwa Kiingereza: “The blindness of that one is his good fortune.”
Methali ina maana sawa na mapito ya msanii Elizabeth Michael ‘Lulu’, kwamba pamoja na uchakaramu wake lakini humohumo mafanikio yake yanapatikana. Hongera zake kwa tuzo aliyotwaa Nigeria.
Tuzo ya Lulu ina maana ya hatua tatu ambazo amezipitia kwenye tasnia ya sanaa za maigizo nchini. Na bila shaka, Lulu bado anaidai fedha nyingi tasnia hiyo.
SANAA KIMEO
Lulu alianza kuigiza akiwa mtoto mdogo kabisa. Uwezo wake wa kuigiza ulionekana. Kipaji kikubwa cha sanaa za maigizo ni ngao inayombeba Lulu tangu alipokuwa anachipukia Kundi la Kaole Sanaa kisha michezo yao kurushwa televisheni za ITV na baadaye TBC1.
Sanaa ilimharibu Lulu, maana watayarishaji walimpangia maeneo ya kucheza kama mtoto mtukutu, na waongozaji walifanya kazi yao vizuri kuhakikisha Lulu anaimudu nafasi husika.
Wanasaikolojia wanaeleza kuwa mtoto huharibika kwa kuona kwa macho. Lulu alikuwa kwenye kambi za Kaole na akawa anajionea jinsi wasanii wenye umri mkubwa wakifanya mazoezi ya uhusika wa kimapenzi, usaliti, kuumizana na ndoa.
Vilevile kwa kuigiza tabia mbaya (mtoto mtukutu) kama alivyokuwa akiigiza, taratibu vitabia hivyo vya kuigiza vilikuwa vikiingia kwenye mzunguko wa maisha yake na kujitengeneza kama tabia yake halisi.
Wataalam wa saikolojia katika somo la Problematic Psychology, wanaeleza kuhusu hatari za wasanii kuwa watu waovu kutokana na maeneo wanayoigiza katika filamu, tamthiliya au michezo yoyote ya kuigiza.
Ongeza mfano; Martin Lynes, 48, aliyeigiza kama mhalifu wa kwenye nyumba za watu katika kipindi maarufu cha maigizo nchini Australia cha Home and Away, hivi sasa yupo matatani, akituhumiwa kumbaka mwanamke mwenye umri wa miaka 51, kumpiga na kumuumiza.
Hapo unaweza kuona mfano wa Lynes, yaliyomtokea Lulu na walichokisema wanasaikolojia.
SANAA NUSURA IMPOTEZE
Kimsingi sanaa ya Tanzania ilimkuza kuliko umri wake. Ghafla akadaiwa kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na wanaume wakubwa, yeye akiwa na umri chini ya miaka 18.
Ilikuwa lazima iwe hivyo kwa sababu aliyaona mapenzi waziwazi akiwa kazini na aliyatamani, ndiyo maana aliyawahi.
Na hiyo siyo kwa Lulu tu, wasanii wengi waliopata mafanikio wakiwa na umri mdogo, hukimbilia sana mapenzi. Bow Wow, alipokaribia miaka 18 alisema: “Nikifikisha umri wa miaka 18 naoa, nitakuwa sina kizuizi, umri utakuwa unatosha na pesa ninayo.”
Hapa ni kuonesha kuwa Bow Wow alikuwa anayatamani sana mapenzi kwa uhuru, na ni sawa tu kusema alikuwa anashughulika nayo sirisiri. Alikuwa akiyaona kwa wakubwa, viwanja akienda, akiwa katika maeneo ya kurekodia, akawa anayatamani sana.
Lulu akaripotiaw kulewa mpaka chakali, akahusishwa na watu kadhaa kimapenzi, kifo cha Steven Kanumba ‘The Great’ kikaondoa shaka yote ya ushiriki wake wa kimapenzi katika umri mdogo.
Yupo mtu ambaye anaweza kudhani kifo cha Kanumba ndiyo nusura kimpoteze Lulu, hapana! Kifo cha Kanumba angalau kimemsaidia. Kimempunguzia ile kasi aliyokuwa nayo. Angalau hofu imekuwepo.
Lulu tangu ametoka jela, hajawahi kuripotiwa kulewa mpaka kuzimika akiwa viwanja. Ni ukweli kuwa kifo cha Kanumba kimembadilisha.
SANAA SASA INAMNG’ARISHA
Tuzo aliyopata Nigeria anastahili. Lulu ni mkongwe japo umri wake mdogo. Ana umri mkubwa kwenye game kuliko wasanii wengi wanaotamba kwa sasa. Na kipindi chote amekuwa fundi wa kuigiza. Ana uwezo mkubwa!
Hatimaye sanaa iliyomharibu, ikataka kumpoteza, sasa inamvusha boda mpaka Nigeria kisha anabeba tuzo kwenye nchi za watu na kurudi nayo nyumbani.
Muhimu ni kuwa anastahili kuendelea kufanya kazi nzuri kwa sababu jina analo, mashabiki anao, kipaji anacho na fursa anazo, ni jukumu lake kuutumia muda wake wa sasa kutengeneza fedha.
Hongera Lulu, hongera Single Mtambalike ‘Richie’ kwa kuiwakilisha vema nchi kwenye tuzo za Africa Magic Viewers Choice Awards (AMVCA) 2016. Mliteuliwa na mmeshinda.
Hata Richie, sanaa hii bado anaidai fedha nyingi maana ameitoa mbali. Amesafiri nao kuvuka mabonde na milima. Ni haki kabisa kwa mtu ambaye amehangaikia fani yake ikamlipa inavyotakiwa. Richie anastahili pia tuzo yake.




Share on Google Plus

About LUQMAN MALOTO

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment