Mama Moses ni mwanamke wa kimjinimjini, alianza kuwajua
wanaume mapema sana. Akiwa na umri wa miaka 16, alipewa ujauzito na jamaa
aliyekuwa kondakta wa daladala kwa wakati huo. Hakuwa na jinsi alijifungua
mtoto wa kiume, akamwita Moses.
Kwa sasa Mama Moses ana umri wa miaka 44, Moses ana miaka
28. Mtu na mwanaye wanaishi kama wazungu. Maisha yao si haba, kwani miaka 19
iliyopita, Mama Moses alimliza mzungu mmoja kiasi kikubwa cha fedha, baada ya
hapo akawekeza kwenye biashara mbalimbali, ikiwemo maduka Kariakoo na akawa
anafuata mizigo China.
Moses ni mtoto wa pekee, kwa hiyo maisha yake yakawa
kutumbua fedha za mama yake. Alizitumia kuendesha magari makali akiwa na umri
mdogo kabisa. Alihakikisha anatoa ule mkong’oto wa baba na mama kwa warembo
tofautitofauti, ikiwemo wanafunzi.
Hakuishia hapo, Moses alibeba mpaka mizigo inayomzidi kimo. Alitoka
kimapenzi na wanawake wenye umri kumzidi hata mama yake. “Ninapopata jimama la
ukweli, lililonizidi umri nainjoi sana. Hawa watoto nimewazoea, hawanipi stimu
kabisa,” Moses aliwahi kumwambia rafiki yake Slay.
Kwa upande mwingine, Mama Moses tangu afikishe umri wa miaka
40, hakutaka kabisa kushiriki mapenzi na wanaume wenye umri mkubwa zaidi yake.
“Zamani nilikuwa natembea na mibaba ili nipate fedha, sasa hivi hela ninayo,
nataka vijana tu wanipe raha,” hiyo ni kauli ya Mama Moses, akimwambia shosti
wake Monica.
“Hivi wewe Moses huwezi kuangalia warembo wa saizi yako?
Tabia gani ya kutembea na mimama mikubwa, tena mingine inaweza hata kunizaa,”
Mama Moses aliwahi kumwonya mwanaye.
“Mama wewe ndiye unanikata stimu, unatoka na vijana wadogo
saizi yangu, wengine hata mimi nawazidi umri,” Moses alimjibu mama yake. Pamoja
na hivyo, hakuna kati yao aliyekoma.
Kuna siku moto uliwaka nyumbani kwao. Mama mtu alianza
kumtuhumu mwanaye kuwa ametembea na rafiki yake Monica. “Wewe Monica si ni mama
yako kabisa? yule ni rafiki yangu wa siku nyingi, wewe unajua lakini umetembea
naye bila woga,” Mama Moses alimuwakia Moses ambaye naye alijibu: “Kweli mama
mkuki kwa nguruwe, wewe ulifurahi sana ulipotoka na mshakaji wangu Aslay.”
Maisha yalizidi kwenda kasi, siku moja Moses akiwa klabu na
marafiki zake, mara Jaca ambaye ni mshakaji wake mwingine aliingia. Walipiga
stori mbalimbali lakini katikati ya mazungumzo, mmoja wa marafiki wa Moses
alimuuliza Jaca ni kwa nini alichelewa klabu?
Jaca akajibu: “Leo jionijioni nilikutana na bonge la jimama,
likanizimia halafu lina mawe kinoma, nikaona siyo vibaya ngoja nijiweke.
Tulikula bata, tukaziua bia kama tumerogwa vile, baada ya hapo tukazama zetu
chumbani kwenye hoteli moja hapo kati.
“Kabla ya kuanza mambo, machale yakanicheza. Ikabidi
nimsimamie yule jimama aendelee kunywa, alewe ili nimtoroke. Alipolewa
nikamkimbia zangu ndiyo maana mnaona nimechelewa. Maradhi mengi jamani, ukimwi
upo.”
“Acha uzembe wewe, kwani hakuna kondomu?” Moses alimjibu
Jaca. Papo hapo akaomba aelekezwe hoteli na chumba ambacho amemwacha huyo bi. mkubwa.
Maelekezo yalifanyika, Moses ikabidi ajipe stimu kwa kupiga pombe za kutosha
ndiyo amvae jimama aliyeogopwa na Jaca.
Baada ya kujitwika pombe za kutosha, Moses aliongozana na
Jaca mpaka hotelini, wakapanda ghorofani mpaka kwenye chumba husika. Jaca
aliingia kwanza kuhakikisha mazingira yapo salama, alipojiridhisha, alizima
taa, halafu akatoka nje.
“Sasa wewe ukiingia ndani, anza kazi. Mama yupo hoi,
usiwashe taa atakushtukia mapema,” Jaca alimpa maelezo Moses ambaye aliyapokea
kisha akaingia ndani. Alipofika tu, alisoma gizani na kujua mahali kitanda
kilipo na bi. mkubwa akiwa amejaa tele.
Akavua nguo harakaharaka, kisha akahamia kwa yule bi.
mkubwa, akamchojoa kiwalo kimoja baada ya kingine. Alipofikia usawa wa kufuli,
jimama lilijigeuza kama mzigo kisha akazungumza kwa sauti ya pombe: “Safi baby,
unataka kunipa raha.”
Moses wala hakujibu, alichokifanya kwa wakati huo ni
kumwandaa bi. mkubwa, tayari kwa shughuli inayofaa eneo walilopo. Jimama akawa
anahangaika huku na huko, pombe zikawa zinamezwa na ule mchezo aliokuwa
anafanyiwa. Mwisho mechi ikaanza.
Ilikuwa mechi yenye kila aina ya kashkashi za utamu kwa
pande zote mbili. Moses alijitahidi kucheza salama, kila baada ya mchakamchaka
mfupi, alichomoa daruga kuhakikisha kama kiatu kipo, kimevuka au kimepasuka.
Aliporidhika kipo aliendelea kwa ari, nguvu na kasi zaidi.
Baada ya mchuano, wote walipitiwa na usingizi. Palipokucha,
mwanga ukiwa umeshaingia chumbani, yaani siyo giza tena, Moses ndiye alikuwa wa
kwanza kuamka. Akakumbuka matukio ya usiku uliopita, pombe zilishamwisha,
akamwangalia jimama aliyepata naye raha usiku mzima.
“My God,” Moses alijikuta akitamka maneno hayo kwa mshangao.
Ni maneno hayohayo ndiyo yaliyomwamsha yule bi. mkubwa ambaye mpaka wakati huo,
alikuwa hana nguo hata moja.
Macho yakawatoka wote wawili, hakuna aliyethubutu kufungua
kinywa kuzungumza chochote, kwani yule bi. mkubwa hakuwa mwingine, bali ni Mama
Moses, kwa hiyo mama na mwana walipeana huduma ya faragha usiku mzima bila
kujuana.
SHIKA HII
Ni vizuri kujiheshimu. Umakini unahitajika kila wakati.
0 comments :
Post a Comment