ads 728x90 B

Wabunge wanakula rushwa! Hongereni kwa kazi nzuri!



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEipiJeYIazwJm9_VpBipUqkPRBbDkzjQ07K8eWfbYp7T-h_u132E0CoZRZzmmcFZXu0u12khpg1k7knXaJAUXa0C_TydICRVEzMijE6jltcmaA3LlcUMJVsyRygecGEwd4iUQmpjjf5KJw/s1600/3-naibu+spika+wa+Bunge+Job+Ndugai+akifafanua+miongozo+mbalimbali+Buungeni+leo-742501.JPG
Na Luqman Maloto
KAMA wabunge wanakula rushwa. Tazama malipo yao, daraja wanalopewa, vipi tafriki barabarani?
Mbunge aliyesema gari la shilingi milioni 90 halifai, vipi nesi ambaye mshahara wake wa mwezi haukidhi japo mzunguko wa wiki?
Nidhamu hakuna kabisa. Wabunge na heshima zao wanatuhumiwa kuomba rushwa. Acha Rais John Magufuli achukue pointi zake.
Na hapa ni kuwa kivuli cha Rais Magufuli kinaonekana kutokana na tukio tukio la kashfa kubwa za rushwa bungeni.
Tayari wabunge Zitto Kabwe, Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo) na Hussein Bashe, Nzega Mjini (CCM) wamejiuzulu ujumbe wa kamati ya bunge kutokana na kashfa ya rushwa.
Uamuzi wa Zitto na Bashe, ni kufuatia habari kuwa Spika wa Bunge, Job Ndugai amefanya mabadiliko ya kamati za bunge kutokana na kashfa za rushwa.
Zitto na Bashe wamejiuzulu na kutaka uchunguzi ufanyike ili wahusika wachukuliwe hatua. Wamekataa kuwa wajumbe kwenye kamati yenye wajumbe wenye kashfa ya rushwa.
WALIODAIWA KUNASWA
Imeelezwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Martha Mlata ameshaondolewa kwenye nafasi hiyo. Mlata ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Singida.
Wengine ni Mbunge wa Sumve (CCM), Richard Ndassa wa Kamati ya Uwekezaji na Mitaji, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mbeya, Mary Mwanjelwa ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira.
Wapo makamu wenyeviti na kamati zao ambao ni Raphael Chegeni (Huduma za Maendeleo ya Jamii), Kangi Lugola (Kamati ya Hesabu za Seikali za Mitaa ‘Laac’)
INAMPA TURUFU MAGUFULI
Kwa nini imekuwa mapema sana? Na mbona kashfa zimeripotiwa kwa sehemu kubwa? Jibu ni moja tu, mabadiliko katika mfumo wa uongozi ambao Dk. Magufuli ameyaweka.
Picha ya sasa inaonesha kuwa huko nyuma wabunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kamati zao, walikuwa wakicheza mchezo wa kulinda maovu ya mashirika ya umma.
Kwamba wabunge kupitia kamati zao, wanabaini maovu ya mashirika ya umma, hivyo wabunge wanaomba rushwa ili wasililipue shirika husika.
Katika moja ya vikao vya bunge katika Bunge la 10, aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, aliwahi kuwataja wabunge wawili kumuomba rushwa mkurugenzi mmoja wa halmashauri.
Kafulila alisema kuwa wabunge, Omar Baduel wa Bahi na Godfrey Zambi wa Mbozi Mashariki, wote CCM (sasa Mkuu wa Mkoa wa Lindi), walimshawishi mkurugenzi mmoja wa halmashauri kuwapa rushwa ili wamlinde.
Wakati huo, Kafulila, Zambi na Baduel, walikuwa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC).
INA MAANISHA NINI?
Kafulila alizungumza bungeni waziwazi. Maana yake ni kuwa kumbe wapo wabunge ambao huomba rushwa kwenye mashirika ili kuficha maovu.
Na kwa muda mrefu kumekuwa na kelele kuwa wabunge hupenda baadhi ya kamati zinazohusika na ukaguzi au usimamizi wa hesabu za mashirika ya umma na serikali kuu au ile ya Nishati na Madini.
Mwaka 2012, Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nasari, alisema bungeni na kupendekeza: “Mheshimiwa spika, kumekuwa na tabia ya wabunge kupendelea kamati zenye kuhusika na mashirika makubwa, sasa ibadilishwe wale wa kamati ndogondogo ndiyo wawe wajumbe wa kamati zenye kukimbiliwa na wengi.”
TUNAONA NINI SASA?
Mlipuko wa kashfa ya rushwa bungeni una maana kuwa sasa hivi mashirika ya umma na taasisi za serikali kuu kwa jumla, zimebanwa hasa.
Hivyo, kitendo cha mashirika ya umma na taasisi za serikali, kuripoti kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai kuhusu kuombwa rushwa na kamati za bunge, maana yake ni kwamba nidhamu ya watendaji katika mashirika ya umma inaonekana.
Kwamba mchezo wa zamani ni kuwa wabunge walikuwa wakiomba rushwa kwa mashirika ya umma, watendaji wake kwa hofu wanatoa.
Sasa hivi kutokana na nidhamu ambayo imekuwepo na hofu ya kutumbuliwa majibu, vilevile ukaguzi ambao umekuwa ukifanywa, imekuwa sababu ya badala ya kutoa rushwa, waripoti.
Na imebainishwa kuwa kashfa ya rushwa, imebainika baada ya ukaguzi maalum kufanywa na serikali. .
Mwaka 2012, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi, alimwandikia barua aliyekuwa Spika wa Bunge la 10, Anne Makinda, akimweleza kuhusu baadhi ya wabunge kumuomba rushwa ili wasimliopue bungeni kutokana na iliyokuwa kashfa ya mafuta ghafi kwa ajili ya mitambo ya kuzalisha umeme.
 Barua hiyo ilisababisha mjadala mkubwa na baadaye Spika Makinda aliivunja Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini.
Pamoja na kuvunja kamati, spika aliielekeza kamati ya maadili iliyokuwa chini ya Brigedia Jenerali, Hassan Ngwilizi (aliyekuwa mbunge wa Mlalo, CCM) kufanya uchunguzi wa kashfa hiyo.
Katika uchunguzi huo, zilipenya taarifa kuwa baadhi wajumbe waliumbuana kwa mtindo wa “mbona na wewe… mbona na wewe… unakumbuka na wewe.”
Baadaye Spika Makinda alitoa onyo. Hakuna hatua za kinidhamu zilizochukuliwa baada ya ripoti kukabidhiwa kwake. Alisema onyo kali linatosha! 

Share on Google Plus

About LUQMAN MALOTO

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

1 comments :

  1. Sports toto's: Sports toto's (or simply your business) - Sporting 100
    As the name suggests, the sports betting landscape is already saturated with online bookmakers, with the new iPhone 토토 사이트 추천 and iPad app,

    ReplyDelete